Klabu ya Simba imetangaza rasmi kushiriki mashindano ya Cecafa Kagame Cup yatakayoanza kutimua vumbi julai 24 mwaka huu jijini Kigali , Rwanda .
Simba wametoa kauli hiyo hii Leo wakithibitisha ushiriki wa mashindano hayo yatakayo Jumuisha Timu Mbalimbali ukanda wa afrika mashariki na Afrika ya kati.
Miongoni mwa timu shiriki katika mashindano ya mwaka huu ni pamoja na APR na Rayon Sports za Rwanda , Simba na Singida za Tanzania, Vipers , Al Hilal , Gor Mahia , na Kvz ya visiwani Zanzibar.
Simba itatumia mashindano haya kujiandaa na msimu mpya wa 2026-27 unaotarajiwa kuanza kutimua vumbi Tarehe 12 ya mwezi ujao .