Local,Transfer News,Simba

Loemba mambo magumu Simba, kupewa Thank You

Joel JJ By Joel JJ
β€’
11 Jul 2026
Loemba mambo magumu Simba, kupewa Thank You

Safari ya kiungo wa kimataifa wa Congo Brazzaville, Innocent Loemba, ndani ya Simba SC inaelekea kufikia mwisho baada ya taarifa kueleza kuwa klabu hiyo ipo kwenye mchakato wa kuachana naye.

Loemba anatajwa kutokuwa sehemu ya mipango ya kocha mkuu Steve Barker kuelekea msimu mpya, huku benchi la ufundi likiwa kwenye mchakato wa kusafisha na kuunda upya kikosi chenye kuendana na falsafa ya kocha huyo.

Taarifa zinaeleza kuwa Barker hajamuweka Loemba kwenye mpango wake wa muda mrefu, jambo linaloifanya nafasi ya kiungo huyo kuendelea kubaki Msimbazi kuwa ngumu zaidi.

Loemba alitua Simba katika dirisha dogo la usajili akiwa na matarajio makubwa kutokana na uwezo wake wa kucheza nafasi mbalimbali za kiungo. Mwanzo wake ndani ya kikosi cha Wekundu wa Msimbazi ulikuwa wa kuvutia, akionyesha uwezo wa kumiliki mpira, kupiga pasi na kusaidia timu kwenye maeneo ya ushambuliaji.

Hata hivyo, kadri msimu ulivyoendelea, Loemba alianza kupoteza nafasi kwenye kikosi cha kwanza kutokana na ushindani mkubwa uliokuwepo ndani ya timu pamoja na mabadiliko ya mipango ya benchi la ufundi.

Ujio wa Makgalwa Waongeza Ushindani

Moja ya mambo yanayotajwa kuchangia maamuzi ya Simba ni ujio wa winga Keletso Makgalwa kutoka Sekhukhune United, ambaye anatarajiwa kuongeza nguvu na ushindani katika eneo la pembeni na nafasi za ushambuliaji.

Simba imekuwa ikifanya maboresho kadhaa kwenye kikosi chake kuelekea msimu mpya, huku kocha Barker akitaka kuwa na wachezaji wanaoendana na mfumo na mahitaji yake ya kiufundi.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
2h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
5h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
7h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
9h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
11h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
12h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
14h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
17h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’