Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), katika kikao kilichofanyika jijini Dar es Salaam, imepitia taarifa ya mchezo wa fainali ya Kombe la Shirikisho la Benki ya CRDB (CRDB Bank Federation Cup 2026) uliochezwa Julai 4, 2026 katika Uwanja wa Gombani, Pemba, na kutangaza maamuzi kadhaa ya kinidhamu dhidi ya Azam FC na baadhi ya maafisa wake.





