International,Normal News,Al Hilal, Al Merrikh, Local

Al Hilal wapokonywa ubingwa wa Ligi Kuu Sudan

Joel JJ By Joel JJ
β€’
14 Jul 2026
Al Hilal wapokonywa ubingwa wa Ligi Kuu Sudan

Klabu ya Al Hilal imepoteza rasmi ubingwa wa Ligi Kuu ya Sudan msimu wa 2025/26 baada ya Kamati ya Rufaa ya Shirikisho la Soka la Sudan (SFA) kuidhinisha rufaa iliyowasilishwa na wapinzani wao wakubwa, Al Merrikh.

Uamuzi huo umebadili kabisa msimamo wa ligi, ambapo Al Hilal wameondolewa kileleni na kushushwa hadi pointi 18, huku Al Merrikh wakifikisha pointi 21 na kutawazwa mabingwa wapya wa Sudan.

Chanzo cha adhabu hiyo ni matumizi ya Al Hilal ya wachezaji wanane wa kigeni katika mechi dhidi ya Al Merrikh, idadi ambayo ilidaiwa kukiuka kanuni za mashindano. Baada ya kupitia rufaa ya Al Merrikh, Kamati ya Rufaa iliamua kuipa Al Hilal adhabu ya kupoteza mchezo kwa mabao 2-0, hatua iliyobadilisha msimamo wa mwisho wa ligi na kuondoa ubingwa mikononi mwao.

Uamuzi huo umeibua mjadala mkubwa ndani ya soka la Sudan, hasa kutokana na ukubwa wa ushindani kati ya Al Hilal na Al Merrikh, ambao kwa miongo kadhaa wamekuwa wakitawala soka la nchi hiyo. Mara nyingi, ubingwa wa Sudan umekuwa ukiamuliwa kati ya vigogo hao wawili.

Al Hilal walikuwa wameonyesha kiwango bora uwanjani msimu huu, huku pia wakifanya vizuri katika michuano ya CAF Champions League. Hata hivyo, makosa ya kiutawala kuhusu usajili na matumizi ya wachezaji wa kigeni yamefuta mafanikio yao ya uwanjani na kuwagharimu taji la ligi.

Hata hivyo Al Hilal wamekatia rufaa uamuzi huo wakidai wachezaji watatu wanaolalamikiwa walipata uraia wa Sudan kihalali.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
5h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
7h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
9h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
11h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
12h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
14h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
17h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’