Azam FC inatarajiwa kulipa faini ya shilingi milioni 50 baada ya Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kutoa adhabu kufuatia kitendo cha wachezaji na benchi la ufundi kususia kupokea medali za washindi wa pili baada ya fainali ya Kombe la Shirikisho la CRDB Bank.
Hatua hiyo imekuja baada ya Azam FC kuondoka bila kushiriki kikamilifu katika hafla ya utoaji wa medali kufuatia kupoteza mchezo wa fainali dhidi ya Simba SC, uliomalizika kwa ushindi wa bao 1-0.
Kwa mujibu wa uamuzi wa Kamati ya Nidhamu ya TFF, klabu hiyo imepewa adhabu ya faini ya shilingi milioni 50 kutokana na kukiuka taratibu na kanuni za mashindano kwa kususia hafla rasmi ya utoaji wa medali.
Azam FC ina nafasi ya kutekeleza adhabu hiyo au kufuata taratibu za kukata rufaa kama zilivyoainishwa kwenye kanuni za TFF.