International,Normal News,Kombe la Dunia 2026, Michezo, FIFA World Cup 2026

FIFA kutambulisha mpira utakaotumika hatua ya nusu fainali ya Kombe la Dunia 2026

Jairo Mtitu By Jairo Mtitu
β€’
14 Jul 2026
FIFA kutambulisha mpira utakaotumika hatua ya nusu fainali ya Kombe la Dunia 2026

Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) kwa kushirikiana na kampuni ya vifaa vya michezo ya Adidas, wametangaza mpira maalumu utakaotumika kuanzia hatua ya nusu fainali hadi mchezo wa fainali wa Kombe la Dunia 2026.

Mpira huo unaoitwa Trionda Final ni toleo maalumu la mpira wa Trionda uliotumika katika hatua za makundi hadi robo fainali za mashindano hayo. Kwa mujibu wa Adidas, mpira huo umeendelea kubeba teknolojia na muundo wa awali, lakini umeongezewa muonekano mpya unaoendana na ukubwa wa mechi za hatua za mwisho za Kombe la Dunia.

Muundo wa Trionda Final umepewa heshima kwa kuenzi miji itakayokuwa mwenyeji wa hatua za mwisho za michuano hiyo ambayo ni Dallas, Atlanta, Miami na New York/New Jersey.

Mpira huo una mchanganyiko wa rangi za dhahabu, nyeupe na nyeusi, ambapo rangi ya dhahabu inaashiria thamani na hadhi ya Kombe la Dunia la FIFA, huku nyeusi ikiupa muonekano wa kipekee kuelekea mechi za kuwania ubingwa wa dunia.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
8h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
11h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
13h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
15h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
17h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
18h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
18h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
20h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
23h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’