Local,Transfer News,Simba Sc, Yanga

Keletso Makgalwa ni uhakika Msimbazi

Joel JJ By Joel JJ
β€’
14 Jul 2026
Keletso Makgalwa ni uhakika Msimbazi

Klabu ya Simba SC imezidi kuonyesha ubabe katika soko la usajili baada ya kumsajili kiungo mshambuliaji tegemeo wa Sekhukhune United ya Afrika Kusini, Keletso Makgalwa (29), kuelekea msimu mpya wa mashindano.

Taarifa za ndani kutoka ndani ya Msimbazi zinathibitisha kuwa miamba hiyo ya soka nchini imefikia muafaka wa mwisho na klabu ya Sekhukhune United pamoja na mchezaji huyo mwenyewe, huku masuala yote ya kimkataba na maslahi binafsi yakiwa yamekamilika kwa asilimia mia moja.

Kocha Mkuu wa Simba, Steve Barker anatajwa ushawishi wake kufanikisha usajili wa winga huyo ambaye tetesi zinaeleza kuwa alikuwa akiwaniwa na watani zao Yanga ambao kocha wao mpya Manqoba Mngqith ambaye ni raia wa Afrika Kusini alitajwa kufanya mawasiliano na winga huyo kumshawishi bila ya mafanikio

Barker anajua vyema uwezo wa Makgalwa kwani amewahi kufanya naye kazi huko nyuma, ndiye aliyependekeza jina la nyota huyo mwenye kasi na uwezo mkubwa wa kucheza nafasi ya winga wa kushoto na kiungo mshambuliaji wa kati.

Makgalwa amewahi pia kukipiga katika miamba ya soka ya Mamelodi Sundowns, anasifika kwa uwezo wake mkubwa wa kumiliki mpira, kupiga pasi za mwisho, na uzoefu wa michuano mikubwa ya ndani na nje ya Afrika Kusini sifa ambazo benchi la ufundi la Simba linaamini zitakuwa msaada mkubwa katika kurejesha heshima ya klabu hiyo kitaifa na kimataifa.

Uongozi wa Simba SC unatarajiwa kumtambulisha rasmi nyota huyo hivi karibuni, huku kukiwa na matumaini makubwa kuwa usajili huu utaongeza nguvu kubwa katika safu ya ushambuliaji ya Wekundu wa Msimbazi.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
5h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
9h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
11h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
13h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
15h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
15h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
16h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
18h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
21h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’