Local,Normal News,YangaSC, Pre Season

Yanga yathibitisha kambi ya pre-season kufanyika Avic Town, hakutakuwa na safari ya nje

Jairo Mtitu By Jairo Mtitu
β€’
14 Jul 2026
Yanga yathibitisha kambi ya pre-season kufanyika Avic Town, hakutakuwa na safari ya nje

Klabu ya Yanga SC imethibitisha kuwa maandalizi yake ya msimu wa 2026/27 yatafanyika katika kambi ya Avic Town, huku ikieleza kuwa hakutakuwa na safari ya kwenda nje kwa ajili ya mazoezi ya kujiandaa na msimu mpya.

Akizungumza kuhusu maandalizi hayo, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga SC, Ali Kamwe, amesema uongozi wa klabu umefanya tathmini ya ratiba iliyopo na kuamua kubaki Avic Town kutokana na muda mfupi uliobaki kabla ya kuanza kwa mashindano ya msimu mpya.

"Pre-season yetu mwaka huu tunabakia pale pale Avic Town. Hakutakuwa na safari ya kwenda popote kutokana na muda uliobakia," amesema Kamwe.

Kauli hiyo inaweka wazi kuwa kikosi cha Wananchi kitaendelea na programu zake zote za maandalizi katika kambi hiyo, ambapo benchi la ufundi litakuwa na nafasi ya kuwaunganisha wachezaji wapya na wale waliobaki kikosini, sambamba na kuboresha mbinu na utimamu wa mwili kuelekea msimu ujao.

Yanga inaendelea na maandalizi ikiwa na malengo ya kutetea mafanikio yake kwenye mashindano ya ndani na kufanya vizuri zaidi katika michuano ya kimataifa ya CAF, huku mashabiki wakisubiri

Mabingwa hao wa ligi kuu ya Tanzania Bara kwa misimu mitano mfululizo wanatarajiwa kuingia kambini Julai 20

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE β†’