Rais wa heshima wa klabu ya Simba SC, Mohamed "Mo" Dewji, amekutana na Kocha Mkuu wa klabu hiyo, Steve Barker, nchini Afrika Kusini kwa ajili ya kujadili maandalizi ya timu kuelekea msimu mpya wa 2026/27.
Katika kikao hicho, viongozi hao walijadili kwa kina maendeleo ya kambi ya maandalizi, hali ya kikosi, pamoja na mikakati ya kuendelea kukiimarisha ili Simba iwe na ushindani mkubwa katika Ligi Kuu ya NBC, Kombe la Shirikisho la CRDB Bank na michuano ya kimataifa ya CAF.
Pia waligusia umuhimu wa kuwajenga wachezaji katika viwango vya juu vya ushindani, kuhakikisha kikosi kinakuwa na utimamu wa mwili na mbinu sahihi kabla ya kuanza kwa msimu mpya.
Uongozi wa Simba unaendelea kusisitiza dhamira ya kuunda timu imara itakayopambania mataji yote inayoshiriki.
Mkutano huo unaonyesha ushirikiano wa karibu kati ya uongozi na benchi la ufundi katika kuhakikisha Simba inaingia msimu mpya ikiwa imejiandaa kikamilifu na yenye malengo makubwa ya kufanya vizuri ndani na nje ya Tanzania.