Local,Transfer News,Simba Sc, Wydad

Mwalimu aongeza mkataba wa mkopo Simba

Joel JJ By Joel JJ
β€’
15 Jul 2026
Mwalimu aongeza mkataba wa mkopo Simba

Klabu ya Simba SC imefanikiwa kuongeza muda wa huduma ya mshambuliaji wake Suleiman Mwalimu Gomez baada ya kufikia makubaliano mapya na klabu ya Wydad AC ya Morocco kuhusu mkataba wa mkopo wa msimu mzima.

Kwa mujibu wa taarifa, Mwalimu ataendelea kuvaa jezi ya Simba katika msimu wa 2026/27, huku klabu hiyo ikiendelea kunufaika na uwezo wake wa kufunga mabao na kusaidia safu ya ushambuliaji.

Mshambuliaji huyo ameamua kusalia Msimbazi baada ya kuonyesha kiwango bora katika msimu wake wa kwanza, licha ya kuwepo kwa tetesi zilizomuhusisha na kuwindwa na wapinzani wa ndani zikiwemo Azam FC na Yanga SC.

Mwalimu alijiunga na Simba msimu uliopita kwa mkopo akitokea Wydad AC, na haraka akawa sehemu muhimu ya mipango ya benchi la ufundi kutokana na uwezo wake wa kumalizia mashambulizi.

Katika msimu uliopita, Mwalimu alikuwa mfungaji bora wa Simba kwenye mashindano yote, akifanikiwa kufunga mabao 15, rekodi iliyowafanya mabosi wa Simba warudi tena Morocco kwa waajiri wake Wydad kurefusha mkataba wake wa mkopo.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE β†’