Local,Normal News,Tanzania, Serengeti Boys, Tanzanite Queens

Serengeti Boys Walamba Milioni 500, Tanzanite Queens Wapokea Milioni 50

Jairo Mtitu By Jairo Mtitu
β€’
15 Jul 2026
Serengeti Boys Walamba Milioni 500, Tanzanite Queens Wapokea Milioni 50

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limezikabidhi zawadi za fedha kwa timu za taifa za vijana kufuatia mafanikio yao makubwa katika mashindano ya kimataifa.

Serengeti Boys wamekabidhiwa Shilingi milioni 500 baada ya kufuzu kwa mara ya kwanza kwenye Fainali za Kombe la Dunia la FIFA zitakazofanyika nchini Qatar, sambamba na kutinga fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON U-17) nchini Morocco.

Kwa upande wa Tanzanite Queens, wamepokea Shilingi milioni 50 ikiwa ni pongezi kwa kufuzu kushiriki Fainali za Kombe la Dunia la Wanawake chini ya miaka 17, zitakazofanyika mwezi Septemba mwaka huu nchini Poland.

TFF imeeleza kuwa zawadi hizo ni kutambua juhudi, uzalendo na mafanikio ya wachezaji, benchi la ufundi na viongozi wa timu hizo, huku ikisisitiza dhamira yake ya kuendelea kuwekeza katika maendeleo ya soka la vijana nchini.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
8h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
11h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
13h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
15h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
17h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
18h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
18h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
20h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
23h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’