Klabu ya Singida BS imethibitisha kumrejesha mshambuliaji wake wa zamani Jonathan Sowah akitokea klabu ya Simba.
Taarifa iliyotolewa na Singida BS, imebainisha kuwa Sowah amerejea tena kunako klabu hiyo baada ya kipindi kifupi cha kuwatumikia Wekundu wa Msimbazi.
Nyota huyo raia wa Ghana amesaini mkataba wa miaka mitatu utakaomuweka Singida hadi mwaka 2029.





