International,Transfer News,Libya, Senegal, Azam, Yanga, Simba, NBC LEAGUE

Aliyekuwa Kocha wa Azam FC, Ateuliwa Kuinoa Libya

Abdulrahman Said By Abdulrahman Said
16 Jul 2026
Aliyekuwa Kocha wa Azam FC,  Ateuliwa Kuinoa Libya

Kocha wa zamani wa Azam FC, Youssoupha Dabo, ameteuliwa rasmi kuwa kocha mkuu mpya wa Timu ya Taifa ya Libya kwa mkataba wa mwaka mmoja. Shirikisho la Soka la Libya limethibitisha uteuzi huo, likimkabidhi jukumu la kuiongoza timu hiyo kuelekea mashindano yajayo ya kimataifa.

Dabo anachukua mikoba hiyo akiwa tayari anaifahamu vyema timu ya taifa ya Libya, baada ya kuwahi kuwa kocha msaidizi chini ya Aliou Cissé. Kabla ya uteuzi huo, kocha huyo raia wa Senegal amepata uzoefu mkubwa barani Afrika kupitia vilabu vya Teungueth FC, ASC Jaraaf, Azam FC ya Tanzania na AS Vita Club ya DR Congo, sambamba na kuinoa timu ya taifa ya Senegal chini ya umri wa miaka 20.

Jukumu kubwa la Dabo sasa litakuwa kuijenga upya Libya na kuiongoza katika harakati za kufuzu fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027. Uongozi wa Shirikisho la Soka la Libya unaamini uzoefu wake katika ngazi ya klabu na timu za taifa utasaidia kuirejesha timu hiyo katika ushindani wa soka la Afrika.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
4h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
8h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
9h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
11h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
14h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
14h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
14h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
16h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
20h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →