Golikipa Hussein Masalanga amejiunga rasmi na Geita Gold FC, baada ya kukamilisha uhamisho wake kuelekea klabu hiyo kwa ajili ya msimu mpya wa mashindano.
Masalanga alikuwa akiitumikia Young Africans SC kwa mkopo akitokea Singida Black Stars, ambapo alipata nafasi ya kuwa sehemu ya kikosi cha mabingwa hao wa Tanzania Bara na kuongeza uzoefu katika kiwango cha juu cha ushindani.





