Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) limetangaza kuwa fainali ya Kombe la Dunia 2026 itakuwa na onesho rasmi la burudani wakati wa mapumziko, ikiwa ni mara ya kwanza katika historia ya mashindano hayo kuanzisha utaratibu huo.
Kwa mujibu wa FIFA, onesho hilo litafanyika wakati wa mapumziko ya kipindi cha kwanza na linatarajiwa kudumu kwa takribani dakika 11.





