Local,Transfer News,Singida Black Stars

Singida Bs Wafikia makubaliano na mashine ya ‘BundesLiga’ Marcel Canadi.

Xtra 90 Media By Xtra 90 Media
16 Jul 2026
Singida Bs Wafikia makubaliano na mashine ya ‘BundesLiga’ Marcel Canadi.

Klabu ya Singida Black Stars imefikia makubaliano ya kumsajili kiungo mshambuliaji Marcel Canadi (28) raia wa Austria, katika hatua ya kuendelea kuimarisha kikosi chake kuelekea msimu mpya wa mashindano.

Taarifa zinaeleza kuwa pande zote mbili zimekubaliana kusaini mkataba wa muda mfupi wa miezi sita, huku nyota huyo akitarajiwa kujiunga na kikosi hicho mara baada ya kukamilika kwa taratibu za mwisho za usajili.

Canadi si jina geni katika soka la Ulaya, kwani aliwahi kuitumikia Borussia Mönchengladbach II ya Ujerumani, ambako alipata uzoefu mkubwa kabla ya kuendelea na safari yake katika vilabu mbalimbali barani humo.

Uongozi wa Singida Black Stars unaamini kuwa uwezo wa Canadi wa kucheza nafasi mbalimbali za ushambuliaji utaongeza ushindani ndani ya kikosi na kukipa nguvu zaidi kuelekea msimu wa 2026/27.

Iwapo kila kitu kitakwenda kama kilivyopangwa, Marcel Canadi atakuwa mmoja wa nyota wapya watakaovaa jezi ya Singida Black Stars, huku mashabiki wakisubiri kuona mchango wake katika Ligi Kuu Tanzania Bara.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
5h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
9h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
11h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
13h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
15h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
15h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
16h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
18h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
21h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →