Polisi Tanzania FC imefanikiwa kurejea Ligi Kuu ya NBC kwa msimu wa 2026/27 baada ya kuiondoa Tanzania Prisons katika mchezo wa mtoano. Licha ya kufungwa bao 1-0 katika mchezo wa marudiano uliochezwa leo Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya, Polisi Tanzania walifuzu kwa ushindi wa jumla wa mabao 4-1, wakinufaika na ushindi wa mabao 4-0 walioupata katika mchezo wa kwanza.





