International,Normal News,Vincic, Argentina, Spain, WC2026, Messi, Lamine Yamal

Vincic wa Slovenia kusimamia vita ya ubingwa wa Dunia, Hispania dhidi ya Argentina

Abdulrahman Said By Abdulrahman Said
β€’
17 Jul 2026
Vincic wa Slovenia kusimamia vita ya ubingwa wa Dunia, Hispania dhidi ya Argentina

Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) limemtangaza rasmi mwamuzi kutoka Slovenia, Slavko Vini, kuwa msimamizi wa mchezo wa fainali ya Kombe la Dunia 2026 utakaowakutanisha Hispania na Argentina. Fainali hiyo itachezwa Jumapili, Julai 19, 2026, katika Uwanja wa MetLife, New Jersey, Marekani, kuanzia saa 4:00 usiku.

Vini, mwenye umri wa miaka 46, ni mwamuzi wa kimataifa wa FIFA tangu mwaka 2010 na anatajwa kuwa miongoni mwa waamuzi wenye uzoefu mkubwa katika soka la kimataifa. Katika kipindi chake cha uamuzi, amechezesha mechi nyingi za hadhi ya juu katika mashindano ya FIFA na UEFA.

Miongoni mwa mechi kubwa alizowahi kusimamia ni fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya mwaka 2024 kati ya Real Madrid na Borussia Dortmund, pamoja na michezo ya Kombe la Dunia la Klabu 2025 lililofanyika nchini Marekani. Uzoefu huo umechangia FIFA kumpa jukumu la kusimamia fainali ya mashindano makubwa zaidi ya soka duniani.

Uteuzi wa Vini unakuja huku dunia ikisubiri kwa hamu pambano la fainali kati ya Hispania na Argentina, ambapo mataifa hayo mawili yatapambana kuwania taji la Kombe la Dunia 2026 katika mchezo unaotarajiwa kuvuta hisia za mamilioni ya mashabiki duniani.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
5h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
9h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
11h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
13h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
15h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
15h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
15h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
17h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
21h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’