Local,Transfer News,Azam Fc, Lupopo

Molia atambulishwa Azam FC

Joel JJ By Joel JJ
18 Jul 2026
Molia atambulishwa Azam FC

Klabu ya Azam FC imekamilisha usajili wa kiungo mshambuliaji Enock Molia kutoka FC Saint-Éloi Lupopo ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ikiwa ni sehemu ya mipango ya kuimarisha kikosi kuelekea msimu mpya wa mashindano.

Molia ambaye anatajwa kuwa miongoni mwa wachezaji waliokuwa na kiwango bora katika Ligi Kuu ya DR Congo, amefanikiwa kuvutia viongozi wa Azam FC kutokana na uwezo wake wa kucheza eneo la pembeni la ushambuliaji, kasi pamoja na uwezo wa kutengeneza nafasi na kufunga mabao.

Taarifa zinaeleza kuwa nyota huyo wa Congo amesaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia Azam FC, huku akitarajiwa kuleta nguvu mpya katika safu ya ushambuliaji ya timu hiyo inayolenga kufanya vizuri katika mashindano ya msimu ujao.

Usajili wa Molia unaendana na mkakati wa Azam FC wa kuongeza ubora wa kikosi chake kwa kusajili wachezaji wenye uwezo wa kuleta tofauti ndani ya uwanja. Awali, kocha Florent Ibenge alitajwa kuvutiwa na huduma ya mchezaji huyo kutokana na sifa zake za kushambulia na uwezo wake wa kuendana na mfumo wa timu.

Katika msimu uliopita akiwa FC Lupopo, Molia alionyesha kiwango kizuri na kuwa mmoja wa wachezaji muhimu wa klabu hiyo, huku akihusika kwenye kutengeneza na kufunga mabao.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
5h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
9h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
11h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
13h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
15h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
15h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
16h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
18h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
21h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →