Baada ya wiki kadhaa za burudani, mabao ya kuvutia na mechi zenye ushindani mkubwa, Kombe la Dunia 2026 linafikia tamati huku macho ya dunia yakielekezwa si tu kwenye bingwa mpya, bali pia kwa washindi wa tuzo binafsi za FIFA zitakazotolewa mara baada ya fainali.
Tuzo zinazosubiriwa kwa hamu ni Golden Ball kwa mchezaji bora wa mashindano, Golden Boot kwa mfungaji bora, Golden Glove kwa golikipa bora na Best Young Player kwa nyota bora chipukizi aliyeangaza zaidi katika michuano hiyo.
Mbio za Golden Boot zinaendelea kuwa kali kabla ya fainali. Nahodha wa Ufaransa Kylian Mbappé anaongoza akiwa na mabao 10, akifuatiwa na Lionel Messi mwenye mabao 8, huku Jude Bellingham akiwa na mabao 7. Harry Kane amefunga mabao 6, wakati Mikel Oyarzabal wa Hispania akifikisha mabao 5 na bado ana nafasi ya kuongeza idadi hiyo kwenye mchezo wa mwisho.
Kwa upande wa Golden Ball, ushindani ni mkali kati ya nyota walioiongoza timu zao kufika hatua za mwisho za mashindano. Maonyesho ya Messi, Mbappé na Oyarzabal yamekuwa kivutio kikubwa, huku mchango wao wa mabao na pasi za mwisho ukiwa muhimu kwa mafanikio ya timu zao.
Tuzo ya Golden Glove nayo inatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kati ya makipa walioonyesha ubora mkubwa katika mechi za mtoano, huku Best Young Player ikionekana kuwa vita ya nyota chipukizi waliotikisa mashindano kwa kiwango chao na kuonyesha kuwa wao ndiyo kizazi kijacho cha soka la dunia.
Wewe unadhani nani ataondoka na tuzo hizi?
- Golden Ball
- Golden Boot
- Golden Glove
- Best Young Player.