Local,Normal News,Simba sc

Simba wamepata upgrade ya Mzamiru Yassin kupitia Kelvin Nashon.

Xtra 90 Media By Xtra 90 Media
β€’
20 Jul 2026
Simba wamepata upgrade ya Mzamiru Yassin kupitia Kelvin Nashon.

Usajili wa Kelvin Nashon unaonekana kuwa hatua ya Simba SC kuimarisha zaidi safu ya kiungo baada ya miaka ya mafanikio ya Mzamiru Yassin.

Ingawa Mzamiru ameondoka akiwa mmoja wa viungo bora kuwahi kuitumikia Simba, Nashon anaingia akiwa na sifa zinazomfanya aonekane kama upgrade katika baadhi ya maeneo ya kiufundi na kimwili.

MZAMIRU YASSIN

Aliitumikia Simba kwa takribani miaka 10, alicheza zaidi ya mechi 250 katika mashindano yote, alishinda mataji kadhaa ya Ligi Kuu Tanzania, Kombe la FA na Ngao ya Jamii, aliisaidia Simba kufika robo fainali ya CAF Champions League (2021).

Alijulikana kwa nidhamu kubwa uwanjani, uzoefu na uongozi, uwezo wa kukaba na kuzuia mashambulizi, kushinda mipira ya pili na kucheza kwa kujituma dakika zote 90.

KELVIN NASHON

Ni kiungo mwenye umri mdogo na nafasi kubwa ya kuendelea kukua.

Ana uwezo mkubwa wakubeba mpira kutoka nyuma kwenda mbele (ball progression), ushinda mipambano ya mmoja dhidi ya mmoja, kukaba kwa nguvu na kufanya high pressing, kupiga pasi za mbele zinazovunja mistari ya wapinzani, kufunika eneo kubwa kutokana na kasi na nguvu alizonazo.

Kelvin Nashon anaingia Simba akiwa na nguvu zaidi kimwili, kasi kubwa ya mchezo na uwezo wa kuchangia mashambulizi kuliko Mzamiru katika hatua hii ya kazi zao. Wakati Mzamiru alikuwa tegemeo kwa uzoefu na utulivu wake, Nashon analeta nguvu mpya, ubunifu wa kusogeza mpira mbele na uwezo wa kucheza mfumo wa kisasa unaohitaji presha kubwa dhidi ya wapinzani.

Kwa mantiki hiyo, Simba haijapata tu mbadala wa Mzamiru Yassin, bali imepata kiungo mwenye uwezo wa kuipeleka timu kwenye kiwango cha juu zaidi huku akibeba majukumu ya kizazi kipya katika eneo la kiungo.

More Stories

Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
3h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
4h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
9h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
9h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
9h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
11h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
15h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
22h ago
READ MORE β†’
Wapinzani wa Simba, Mighty Wanderers kutua nchini leo wakitokea Malawi
Wapinzani wa Simba, Mighty Wanderers kutua nchini leo wakitokea Malawi
1d ago
READ MORE β†’