Klabu ya Azam FC imekamilisha usajili wa mshambuliaji wa kimataifa wa Sudan, John Mano, kutoka klabu ya Al-Akhdar inayoshiriki Ligi Kuu ya Libya. Uhamisho huu unaipatia Azam nyongeza mpya mbele ya kiwanja, ikiwa ni sehemu ya mkakati wao wa kuimarisha kikosi kabla ya msimu mpya wa 2026/27.
Mano si mgeni apa nchini , kwani aliwahi kuja akiwa na Al Hilal ya Sudan chini ya kocha Ibenge, kabla ya kuhamia Al-Akhdar. Kwa mujibu wa taarifa zilizopo, uamuzi wake wa kujiunga na Azam FC unaelezwa kuchangiwa kwa kiasi kikubwa na ushawishi wa kocha wake huyo wa zamani, ambaye sasa yupo Chamazi.
Kuwasili kwa Mano kunatarajiwa kuongeza nguvu na uzoefu wa kimataifa katika mstari wa mbele wa Azam FC, huku klabu hiyo ikiendelea na jitihada za kujenga kikosi chenye ushindani zaidi kuelekea msimu ujao wa ndani na mashindano ya kimataifa.