Klabu ya Yanga SC imemkaribisha rasmi Kagisho Dikgacoi, kocha mwenye asili ya Afrika Kusini, kuwa sehemu ya kikosi cha ufundi cha kocha mkuu mpya Manqoba Mngqithi, akichukua jukumu la kocha wa mipira ya kutenga (Set Piece Coach). Dikgacoi ni miongoni mwa timu ya kiufundi ya Afrika Kusini iliyowasili Jangwani kufuatana na Mngqithi.
Dikgacoi ana historia ndefu ya soka nchini Afrika Kusini, akiwa aliwahi kucheza kwa timu za Golden Arrows, Fulham, Crystal Palace na Cardiff City, huku pia akiwa mchezaji wa kimataifa aliyecheza mechi 54 kwa Timu ya Taifa ya Bafana Bafana. Kabla ya kujiunga na Yanga, alikuwa msaidizi wa kocha katika klabu ya Golden Arrows, akifanya kazi bega kwa bega na Mngqithi.
Kuwasili kwake kunaendana na mkakati wa Mngqithi wa kuleta timu yenye uzoefu wa kimataifa kutoka PSL, ikiwemo pia wataalamu wengine kama Simo Dladla na mchambuzi wa utendaji Yardaan Valodia, huku lengo kuu likiwa ni kuiwezesha Yanga kuendelea kutawala ndani na kushindana vyema katika Ligi ya Mabingwa Afrika msimu ujao.