Dirisha la usajili mara zote limekuwa likiacha mashabiki wa soka midomo wazi kutokana na usajili wa kushtukiza.
Kiungo mkabaji wa Azam FC, Adolf Mtasingwa amejiunga na klabu ya Kaizer Chiefs inayoshiriki ligi kuu ya Afrika Kusini.
Mtasingwa ametua Kaizer Chiefs baada ya makubaliano baina Chiefs na Azam FC. Nyota huyo alikuwa bado ana mkataba wa mwaka mmoja na Azam Fc.
Kaizer Chiefs, maarufu kama Amakhosi, wamekuwa katika mchakato wa kusuka upya kikosi chao ili kurejesha heshima ya klabu hiyo kwenye ukanda wa Kusini mwa Afrika na bara zima kwa ujumla.
Licha ya kukosa nafasi kwenye kikosi cha kocha Florent Ibenge, Mtasingwa anafamika kwenye soka la Tanzania kutokana na uwezo wake mkubwa wa kukata umeme katikati ya uwanja, kulinda safu ya ulinzi, na kuanzisha mashambulizi.
Uwezo wake wa kimbinu ndio kitu kinachovutia klabu kubwa, na Amakhosi wameona kuwa yeye ndiye mtu sahihi wa kuongeza nguvu na muhimili kwenye eneo lao la kiungo.