Dirisha la usajili mara zote limekuwa likiacha mashabiki wa soka midomo wazi kutokana na usajili wa kushtukiza.
Kiungo mkabaji wa Azam FC, Adolf Mtasingwa amejiunga na klabu ya Kaizer Chiefs inayoshiriki ligi kuu ya Afrika Kusini.
Mtasingwa ametua Kaizer Chiefs baada ya makubaliano baina Chiefs na Azam FC. Nyota huyo alikuwa bado ana mkataba wa mwaka mmoja na Azam Fc.





