Local,Transfer News,Yanga Sc, Mashujaa

Yanga yaibomoa Mashujaa FC, yasajili wachezaji watatu

Joel JJ By Joel JJ
β€’
22 Jul 2026
Yanga yaibomoa Mashujaa FC, yasajili wachezaji watatu

Klabu ya Yanga imeendelea kuonyesha nguvu zake katika dirisha la usajili kuelekea msimu wa 2026/2027 baada ya kukamilisha usajili wa beki wa kati Mohamed Mussa kutoka Mashujaa FC.

Mussa, ambaye ana umri wa miaka 22, amesaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia Yanga, huku akitarajiwa kuimarisha safu ya ulinzi ya mabingwa hao wa Tanzania Bara katika msimu ujao.

Taarifa zinaeleza kuwa beki huyo aliamua kujiunga na Yanga licha ya kuvutiwa na ofa kutoka klabu nyingine kubwa, ikiwemo Azam FC, akichagua kuendeleza safari yake ya soka akiwa Jangwani.

Usajili wa Mohamed Mussa unamfanya kuwa mchezaji wa tatu kuhamia Yanga akitokea Mashujaa FC katika dirisha hili la usajili. Tayari klabu hiyo ilikuwa imewatambulisha mshambuliaji Hussein Mihambo pamoja na mlinzi wa pembeni Abdulnasir Gamal , ambao wote wametokea Mashujaa.

Hatua hiyo inaonyesha wazi imani ya Yanga kwa vipaji vilivyoibuliwa na Mashujaa FC, huku ikiongeza ushindani ndani ya kikosi kinachojiandaa kutetea mataji ya ndani na kufanya vizuri katika michuano ya kimataifa msimu wa 2026/2027.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
5h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
11h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
17h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’