Klabu ya Yanga imeendelea kuonyesha nguvu zake katika dirisha la usajili kuelekea msimu wa 2026/2027 baada ya kukamilisha usajili wa beki wa kati Mohamed Mussa kutoka Mashujaa FC.
Mussa, ambaye ana umri wa miaka 22, amesaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia Yanga, huku akitarajiwa kuimarisha safu ya ulinzi ya mabingwa hao wa Tanzania Bara katika msimu ujao.





