Local,Transfer News,Singida BS

Singida Black Stars yamrejesha Benjamin Tanimu

Joel JJ By Joel JJ
23 Jul 2026
Singida Black Stars yamrejesha Benjamin Tanimu

Klabu ya Singida Black Stars imeendelea kujiimarisha kuelekea msimu mpya baada ya kumrejesha beki wa kati wa timu ya taifa ya Nigeria, Benjamin Tanimu, kwa mkataba wa miaka miwili.

Tanimu, mwenye umri wa miaka 23, anarejea Singida Black Stars akitokea klabu ya Maghreb Fès ya Morocco, ambako alicheza baada ya kuondoka Tanzania. Taarifa zinaeleza kuwa mkataba wake mpya na Singida ni wa miaka miwili, huku ada ya usajili ikibaki kuwa siri.

Anatarajiwa kujiunga na kikosi hicho katika kambi ya maandalizi ya msimu mpya nchini Rwanda.

Beki huyo tayari anaifahamu vizuri mazingira ya soka la Tanzania. Kabla ya kujiunga na Maghreb Fès, aliwahi kuzichezea Ihefu FC na baadaye Singida Black Stars, ambapo alionyesha kiwango bora kilichomfungulia milango ya kucheza nje ya nchi.

Kabla ya safari yake ya kimataifa, Tanimu aliichezea Bendel Insurance ya Nigeria, ambako aliibuka kuwa mmoja wa mabeki bora katika Ligi Kuu ya Nigeria. Umhiri wake ulimpa nafasi ya kuitwa katika kikosi cha Super Eagles, timu ya taifa ya Nigeria.

Mbali na kucheza Morocco, Tanimu pia aliwahi kuhusishwa na klabu ya Crawley Town ya England, jambo lililoonyesha jinsi kiwango chake kilivyokuwa kikifuatiliwa na timu mbalimbali.

Kurejea kwake Singida Black Stars kunatajwa kuwa sehemu ya mkakati wa klabu hiyo wa kujenga kikosi imara kitakachoshindana katika Ligi Kuu Tanzania Bara na mashindano mengine ya msimu wa 2026/27.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
5h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
9h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
11h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
13h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
15h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
15h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
16h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
18h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
21h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →