International,Transfer News,Barcelona, Dortmund

Barcelona yatambulisha usajili wa Adeyemi

Joel JJ By Joel JJ
β€’
23 Jul 2026
Barcelona yatambulisha usajili wa Adeyemi

Klabu ya Barcelona imemtambulisha rasmi mshambuliaji wa Ujerumani, Karim Adeyemi, kuwa mchezaji wake mpya baada ya kukamilisha uhamisho wake kutoka Borussia Dortmund.

Adeyemi, mwenye umri wa miaka 24, amejiunga na miamba hiyo ya La Liga kwa mkataba wa miaka mitano utakaomuweka Camp Nou hadi Juni 2031.

Barcelona imelipa euro milioni 22 kama ada ya msingi ya usajili, huku makubaliano yakijumuisha nyongeza (bonasi) zinazoweza kufikisha euro milioni 7 kulingana na mafanikio ya mchezaji na klabu.

Kocha Hansi Flick alihusika kwa kiasi kikubwa katika kushinikiza usajili huo kutokana na kumfahamu Adeyemi tangu walipokuwa pamoja katika timu ya taifa ya Ujerumani. Flick anavutiwa na kasi, uwezo wa kucheza pande zote za ushambuliaji na presha kubwa anayoweka kwa wapinzani anapopoteza mpira.Β 

Adeyemi anatarajiwa kuongeza ushindani kwenye safu ya ushambuliaji ya Barcelona, akitoa chaguo zaidi kwa kocha Flick pamoja na kuwapa mapumziko wachezaji wa pembeni pale itakapohitajika. Pia anaweza kutumika katika nafasi mbalimbali za mbele kutokana na uwezo wake wa kucheza kama winga wa kulia, kushoto au mshambuliaji wa kati.

Changamoto moja inayomkabili mara baada ya kuwasili ni uchaguzi wa namba ya jezi, kwani namba 27 aliyokuwa akiitumia Borussia Dortmund haiwezi kutumika kwa wachezaji wa kikosi cha kwanza Barcelona kutokana na kanuni za La Liga.

Usajili wa Adeyemi ni sehemu ya mkakati wa Barcelona kuimarisha safu yake ya ushambuliaji kuelekea msimu mpya, huku klabu ikiendelea kutafuta njia ya kujenga kikosi chenye ushindani mkubwa ndani na nje ya Hispania.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE β†’