Klabu ya Simba SC imeendelea kuimarisha kikosi chake kuelekea msimu mpya baada ya kumtambulisha rasmi mshambuliaji Ibrahim Doumbia (22), ambaye anajiunga na Wekundu wa Msimbazi akitokea klabu ya AS Korofina ya nchini Mali.
Kwa mujibu wa taarifa, Doumbia amesaini mkataba wa mwaka mmoja wenye kipengele cha kuongeza mwaka wa pili kulingana na makubaliano ya pande zote.





