Local,Normal News,Simba Sc, Mogadishu

Simba, Mogadishu City hakuna mbabe Kagame Cup

Joel JJ By Joel JJ
β€’
25 Jul 2026
Simba, Mogadishu City hakuna mbabe Kagame Cup

Mchezo wa kwanza wa Kundi B katika michuano ya CECAFA Kagame Cup kati ya Simba SC na Mogadishu City FC umemalizika kwa sare ya bila kufungana, huku timu zote zikigawana pointi moja katika mchezo uliokuwa na ushindani mkubwa.

Simba SC chini ya kocha mkuu Steve Barker ilianza mchezo ikiwa na kikosi chenye mchanganyiko wa nyota wengi wapya waliosajiliwa katika dirisha hili la usajili. Wekundu wa Msimbazi walitawala sehemu kubwa ya mchezo, lakini walikumbana na ukuta imara wa ulinzi wa Mogadishu City ambao ulikaa nyuma kwa muda mwingi kuhakikisha lango lao halifungwi.

Katika dakika 15 za mwisho, Simba iliongeza kasi ya mashambulizi baada ya Barker kufanya mabadiliko ya kuwaingiza Clatous Chama, Shomari Kapombe, Anicet Our, Keletso Makgalwa, Ibrahim Doumbia na Jabeer ili kuongeza nguvu eneo la ushambuliaji.

Doumbia alikaribia kuandika bao la ushindi katika dakika za mwisho za mchezo, huku Makgalwa pia akitengeneza nafasi nyingine nzuri, lakini safu ya ulinzi ya Mogadishu City iliendelea kuwa imara na kuondoa hatari zote langoni mwao.

Baada ya matokeo ya michezo ya leo, Jamus FC inaongoza Kundi B ikiwa na pointi tatu baada ya kuifunga Singida Black Stars mabao 2-0 katika mchezo wa awali. Simba SC na Mogadishu City zinafuatia zikiwa na pointi moja kila moja.

Simba sasa itarejea uwanjani Jumanne, Julai 28, kukutana na Jamus FC katika mchezo unaotarajiwa kuwa na presha kubwa kwa Wekundu wa Msimbazi katika harakati za kuwania nafasi ya kufuzu hatua inayofuata.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
6h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
10h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
11h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
13h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
16h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
16h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
16h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
18h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
22h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’