Mahakama ya Usuluhishi wa Michezo (CAS) imepanga kusikiliza Oktoba 8, 2026, rufaa iliyowasilishwa na Shirikisho la Soka la Senegal (FSF), ambalo linapinga uamuzi wa Kamati ya Rufaa ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF) wa kuiondolea Senegal ubingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025.
Senegal inataka CAS kubatilisha uamuzi huo na kuitambua tena kama bingwa halali wa AFCON 2025. Awali, mnamo Machi 17, 2026, Kamati ya Rufaa ya CAF ilitangaza kuiondolea Senegal ubingwa huo na kuukabidhi Morocco, jambo lililoifanya Senegal kuwasilisha rufaa ikidai kuwa uamuzi huo haukuwa wa haki.
Kesi hiyo inatarajiwa kuvuta hisia kubwa barani Afrika, huku uamuzi wa CAS ukisubiriwa kwa hamu kwani unaweza kubadili rasmi historia ya bingwa wa AFCON 2025 ikiwa rufaa ya Senegal itafanikiwa