Real Madrid wamefikia makubaliano kamili na RB Leipzig ya kumsajili winga wa kimataifa wa Ivory Coast, Yan Diomande, katika usajili unaokadiriwa kuzidi €100 milioni.
Makubaliano hayo yamekamilika usiku huu, huku Diomande akitarajiwa kusafiri kuelekea jijini Madrid ndani ya wiki hii kwa ajili ya vipimo vya afya kabla ya kusaini mkataba wa kuitumikia klabu hiyo hadi Juni 2031.





