Local, Simba Sc

Makgalwa awatumia salamu mashabiki Simba, amekuja kazini

Joel JJ By Joel JJ
β€’
27 Jul 2026
Makgalwa awatumia salamu mashabiki Simba, amekuja kazini

Kiungo mshambuliaji wa Simba Keletso Makgalwa juzi alianza kutema cheche zake katika mchezo wake wa kwanza michuano ya kombe la Kagame dhidi ya Mogadishu City ambao ulimalizika kwa matokeo ya suluhu ya bila kufungana.

Akitambulishwa saa chache kuelekea mchezo huo, kocha mkuu wa Simba Steve Barker alimpa nafasi kwenye dakika 15 za mwisho kama ilivyokuwa kwa baadhi ya mastaa wengine wapya kama Ibrahim Doumbia na Jabeer.

Kuingia kwake na wachezaji wengine wa kikosi cha kwanza ambao walianzia nje kwenye mchezo huo, kulibadili kabisa taswira ya mchezo wengi wakiamini kama Barker angewaanzisha pengine Mogadishu City wangeondoka na kapu la mabao.

Akizungumza baada ya mchezo huo Keletso alisema ametua Msimbazi kwa kazi moja tu, kuisaidia timu iweze kushinda mechi, kutwaa mataji na kuhakikisha wanatimiza malengo ya klabu

“Nimekuja Simba kufanya kazi, kupambana kwa ajili ya timu na kushinda mataji. Nitajitolea kwa kila kitu kuhakikisha mashabiki wanafurahia kile nitakachokitoa uwanjani. Subirini muone,” alisema Makgalwa kwa kifupi.

Kiungo huyo fundi ametua Msimbazi akitokea klabu ya Sekhukhune United akiwa ni pendekezo la kocha Steve Barker.

Alikuwa tegemeo kwenye kikosi cha Sekhukhune kutokana na mchango wake mkubwa kwenye mabao ya timu hiyo.

Baada ya kumshuhudia kwa dakika chache, Wanasimba sasa wana matarajio makubwa kwake wakiamini anakwenda kuongeza ubunifu eneo la ushambuliaji na kutengeneza nafasi nyingi za mabao.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
6h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
10h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
11h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
13h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
16h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
16h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
16h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
18h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
22h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’