Twiga Stars wamefanya matembezi ya barabarani (road walk) kama sehemu ya kurejesha utimamu wa mwili, siku moja baada ya kuifunga Afrika Kusini mabao 2-1 katika mchezo wa WAFCON 2026.
Mazoezi hayo ni sehemu ya maandalizi kuelekea mechi zao zinazofuata kwenye mashindano hayo.
Baada ya kuandika historia kwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Afrika Kusini kwenye mchezo wa Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wanawake (WAFCON 2026), wachezaji wa Timu ya Taifa ya Tanzania wanawake, Twiga Stars, leo wamefanya matembezi ya barabarani (road walk) kama sehemu ya programu ya kurejesha utimamu wa mwili.
Mazoezi hayo ya kawaida baada ya mechi yalilenga kuwasaidia wachezaji kuondoa uchovu wa mchezo uliopita na kujiandaa kwa mechi zinazofuata kwenye mashindano hayo yanayoendelea nchini Morocco.
Twiga Stars waliandika ushindi mkubwa dhidi ya Afrika Kusini baada ya mabao ya Diana Msewa na Hasnath Ubamba, matokeo yaliyowapa mwanzo mzuri katika kampeni yao ya WAFCON 2026.