Local, Simba Sc, Sundowns, Transfer News

Mamelodi Sundowns yaongeza ugumu kwa Simba kumpata Maema

Joel JJ By Joel JJ
β€’
28 Jul 2026
Mamelodi Sundowns yaongeza ugumu kwa Simba kumpata Maema

Hatma ya kiungo mshambuliaji Neo Maema ndani ya Simba SC inaendelea kubaki njia panda baada ya mazungumzo ya kumuongeza mkataba kushindwa kuzaa matunda hadi sasa.

Baada ya mkataba wake wa mwaka mmoja kumalizika, uongozi wa Simba ulikuwa na matumaini ya kuendelea kuwa na huduma ya nyota huyo raia wa Afrika Kusini. Hata hivyo, mipango hiyo imekutana na kikwazo kikubwa kufuatia Mamelodi Sundowns kutumia kipengele cha kuongeza miaka miwili kwenye mkataba wa mchezaji huyo.

Taarifa za ndani zinaeleza kuwa kocha wa Simba, Steve Barker, bado anamuhitaji Maema kama sehemu muhimu ya kikosi chake kwa msimu ujao. Kocha huyo anaamini uwezo na uzoefu wa kiungo huyo unaweza kuisaidia Simba katika mashindano ya ndani na kimataifa.

Kutokana na hatua ya Sundowns, Simba italazimika kuingia kwenye mazungumzo mapya na mabingwa hao wa Afrika Kusini endapo itahitaji kuendelea kuwa na Maema. Hata hivyo, mshahara anaouhitaji mchezaji huyo umeonekana kuwa kikwazo kikubwa katika kufikia makubaliano.

Maema ni mmoja wa wachezaji wanaolipwa mishahara mikubwa ndani ya kikosi cha Simba, hali inayoufanya uongozi wa klabu hiyo kutathmini kwa makini kabla ya kufanya uamuzi wa mwisho kuhusu mustakabali wake.

Kwa sasa, kiungo huyo yupo nchini Afrika Kusini, wakati Simba ikiendelea na maandalizi ya msimu mpya kupitia michuano ya CECAFA Kagame Cup inayofanyika Kigali, Rwanda.

Wakati huo huo, Simba tayari imeimarisha safu yake ya ushambuliaji kwa kumsajili kiungo mshambuliaji Ibrahim Jabeer kutoka Stellenbosch FC. Ujio wa Jabeer unaonekana kupunguza presha ya kuhakikisha Maema anabaki Msimbazi, hasa kutokana na gharama kubwa zinazohitajika kukamilisha dili hilo.

Jabeer ana uwezo wa kucheza katika nafasi na majukumu yaliyokuwa yakifanywa na Maema, ingawa Barker bado anatamani kuwa na wachezaji hao wote wawili ndani ya kikosi chake ili kuongeza ushindani na ubora kuelekea msimu mpya.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
59m ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
10h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE β†’