Klabu ya Yanga SC imethibitisha kuwa tamasha la Yanga Day litapambwa na mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Les Aigles du Congo (Samouraïs) kutoka Kinshasa, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Mchezo huo unatarajiwa kuwa sehemu ya kilele cha sherehe hizo, huku mashabiki wa klabu hiyo wakipata nafasi ya kuiona timu yao kabla ya kuanza kwa msimu mpya wa 2026/27.





