Atletico Madrid imekamilisha usajili wa beki wa kimataifa wa Argentina, Cristian ‘Cuti’ Romero, kutoka Tottenham Hotspur, katika usajili unaoipa nguvu safu yao ya ulinzi kuelekea msimu mpya.
Klabu hiyo ya Madrid imethibitisha rasmi leo Jumamosi kwamba Romero amesaini mkataba wa miaka mitano utakaomfanya kuwa mchezaji wa Atlético hadi Juni 30, 2031.





