Raundi ya pili ya Ligi Kuu NBC Premier League 2026/27 inaanza leo Jumanne kwa michezo miwili, huku Mashujaa FC wakiikaribisha Fountain Gate na Geita Gold wakikabiliana na Namungo FC.
Mashujaa wataingia kwenye mchezo huo wakiwa na kumbukumbu ya kuanza msimu kwa ushindi, wakati Fountain Gate wakitafuta kurejea kwenye mstari baada ya kupoteza mchezo wao wa kwanza.





