Azam Fc, Mbeya City zatakata ligi kuu

Joel JJ By Joel JJ β€’ 23rd August 2026


Azam Fc, Mbeya City zatakata ligi kuu

Ligi Kuu ya NBC imeendelea leo zikishuhudiwa mechi mbili za kukata na shoka kwa timu za Azam FC na Mbeya City kuondoka na alama tatu muhimu.

Katika mchezo uliopigwa kwenye Dimba la Azam Complex, Chamazi, wenyeji Azam FC walifanikiwa kuichapa Pamba Jiji mabao 2-1.

Mchezo huo uliokuwa na ushindani mkubwa ulitawaliwa na ufundi mwingi, ambapo magoli ya Azam FC yalipachikwa wavuni na nyota wao Enoch Malia na Abdul Sopu.

Pamba Jiji walijitahidi kupambana na kupata bao la kufutia machozi kupitia kwa Nonyem Okorocha, lakini halikutosha kuwazuia matajiri hao wa viunga vya Chamazi kuondoka na ushindi.

Wakati huohuo, jijini Mbeya ulipigwa mchezo wa mapema ambapo wenyeji Mbeya City wamezinduka na kuibuka kidedea kwa ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Mashujaa FC katika Uwanja wa Sokoine.

Mashujaa FC ndio waliokuwa wa kwanza kuziona nyavu za Mbeya City kupitia goli lililofungwa na Hijja Shamte, goli lilioamsha ari ya wenyeji.

Hata hivyo, Mbeya City walionyesha ukomavu kwa kufanya mapinduzi makubwa (comeback) kipindi cha pili na kusawazisha makosa kupitia mabao ya Adily Buha na Oscar Mwajanga, na hivyo kuwapa mashabiki wa Mbeya burudani na pointi zote tatu nyumbani.


  

More Stories

Azam Fc, Mbeya City zatakata ligi kuu
Azam Fc, Mbeya City zatakata ligi kuu
Today, READ MORE β†’
EPL Updates, Brighton, City mambo mazuri huku Liverpool ikianza na sare.
EPL Updates, Brighton, City mambo mazuri huku Liverpool ikianza na sare.
Today, READ MORE β†’
Bouaddi kurithi mikoba ya Rodri Manchester City
Bouaddi kurithi mikoba ya Rodri Manchester City
Today, READ MORE β†’
Manqoba akiri JKT Tanzania sio ya kubeza
Manqoba akiri JKT Tanzania sio ya kubeza
Today, READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 20, August 23 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 20, August 23 2026
Today, READ MORE β†’
NBC Premier league, Michezo miwili kuendelea.
NBC Premier league, Michezo miwili kuendelea.
Today, READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Hizi hapa ni odds za uhakika, treni la wiki mbili
Xtra 90 Bets : Hizi hapa ni odds za uhakika, treni la wiki mbili
Today, READ MORE β†’
Mourinho aanza na alama tatu La Liga
Mourinho aanza na alama tatu La Liga
Today, READ MORE β†’
Geita Gold yamuangushia Kagera Sugar kipigo cha paka mwizi.
Geita Gold yamuangushia Kagera Sugar kipigo cha paka mwizi.
Yesterday, READ MORE β†’
Highlights : Geita Gold 6-2 Kagera Sugar
Highlights : Geita Gold 6-2 Kagera Sugar
Yesterday, READ MORE β†’