Liverpool wameingia kwenye mbio za kumsajili mshambuliaji wa pembeni wa Crystal Palace, Ismaila Sarr, baada ya kuanza mazungumzo na klabu hiyo kuhusu uwezekano wa kumhamisha mchezaji huyo.
Hatua hiyo imekuja baada ya Liverpool kusitisha nia yao ya kumsajili Yankuba Minteh kutoka Brighton, huku gharama ya uhamisho huo ikitajwa kuwa juu. Kwa mujibu wa taarifa za mtaalamu wa usajili Fabrizio Romano, Liverpool wamewasilisha ofa ya awali ya Pauni milioni 50 kwa ajili ya Sarr.
Crystal Palace, hata hivyo, wanatajwa kutaka kiasi hicho kabla ya kumruhusu mchezaji huyo kuondoka. Sarr, mwenye umri wa miaka 28, alifunga mabao 21 msimu uliopita na alikuwa sehemu muhimu ya kikosi cha Palace katika kampeni yao ya mashindano ya Ulaya pamoja na ushindi wa Community Shield.
Sarr anaripotiwa kuwa tayari kujiunga na Liverpool, ingawa klabu hiyo inakabiliwa na ushindani kutoka kwa Galatasaray, ambao pia wameonyesha nia ya kumsajili mshambuliaji huyo.



