Liverpool wamefikia makubaliano na Paris Saint-Germain (PSG) kwa ajili ya kumsajili winga wa kimataifa wa Ufaransa, Bradley Barcola, katika moja ya dili kubwa linalotarajiwa kukamilika katika dirisha hili la usajili.
Barcola, mwenye umri wa miaka 23, alikuwa tayari amekubaliana masharti binafsi na Liverpool, huku akiripotiwa kuwa na hamu ya kuondoka PSG ili kupata nafasi kubwa zaidi ya kucheza na kuendelea kuimarika katika soka.
Mazungumzo kati ya Liverpool na PSG yaliendelea baada ya klabu hiyo ya Ufaransa kupunguza msimamo wake wa awali wa kutaka ada inayokaribia euro milioni 170, ambayo Liverpool iliona kuwa ni kubwa. Makubaliano yaliyofikiwa sasa yanafungua njia kwa Barcola kuhamia Anfield.
Msimu uliopita, Barcola alifunga mabao 11 katika michezo 29 ya Ligue 1, huku akifunga mabao mawili na kutoa asisti nne katika michezo 16 ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Usajili wake unatarajiwa kuongeza nguvu katika safu ya ushambuliaji ya Liverpool kufuatia kuondoka kwa Mohamed Salah.



