Mwalimu ruksa kuitumikia Yanga, ITC yake yatumwa TFF

Joel JJ By Joel JJ β€’ 28th August 2026


Mwalimu ruksa kuitumikia Yanga, ITC yake yatumwa TFF

Huenda mashabiki wa Yanga leo wakapata nafasi ya kumshuhudia mshambuliaji wao mpya, Seleman Mwalimu, akicheza kwa mara ya kwanza katika kikosi hicho kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania dhidi ya Pamba Jiji.

Yanga itakuwa mwenyeji wa Pamba Jiji leo Ijumaa, Agosti 28, katika mchezo utakaopigwa saa 3:00 usiku kwenye Uwanja wa KMC Complex.

Mwalimu, ambaye usajili wake uliibua gumzo wakati wa dirisha la usajili baada ya Yanga kumnasa kutoka kwenye kambi ya watani wao, Simba SC, alikuwa hajaanza kuitumikia timu hiyo kutokana na kusubiriwa kwa hati yake ya kimataifa ya uhamisho wa mchezaji (ITC).

Hata hivyo, taarifa zinaeleza kuwa suala hilo sasa limepata ufumbuzi baada ya Shirikisho la Soka la Morocco (FRMF) kutuma ITC ya mshambuliaji huyo kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), hatua inayomuweka katika nafasi ya kuanza kuitumikia Yanga.

Iwapo kocha Manqoba Mngqithi ataamua kumtumia, Mwalimu anaweza kuonekana uwanjani leo dhidi ya Pamba Jiji, huku mashabiki wa Yanga wakisubiri kwa hamu kumuona mchezaji huyo mpya akianza safari yake rasmi katika klabu hiyo.

Tofauti na Stephane Aziz Ki, ambaye Mngqithi alisema bado hajawa tayari kucheza, Mwalimu anaonekana kuwa katika nafasi nzuri zaidi kwa kuwa amepata muda wa kutosha wa kufanya mazoezi na timu.

Kabla ya kusajiliwa na Yanga, Mwalimu alikuwa sehemu ya maandalizi ya msimu mpya katika kambi za Simba na Wydad Casablanca, hivyo tayari alikuwa katika programu za mazoezi ya kabla ya msimu (pre-season).


  

More Stories

Barcelona yaichapa Athletic Club 2-0, yarudi kileleni La Liga
Barcelona yaichapa Athletic Club 2-0, yarudi kileleni La Liga
Today, READ MORE β†’
Mwalimu ruksa kuitumikia Yanga, ITC yake yatumwa TFF
Mwalimu ruksa kuitumikia Yanga, ITC yake yatumwa TFF
Today, READ MORE β†’
Simba yatakata Isamuhyo, yaichapa Coastal Union 1-0
Simba yatakata Isamuhyo, yaichapa Coastal Union 1-0
Today, READ MORE β†’
Highlights : Simba 1-0 Coastal Union
Highlights : Simba 1-0 Coastal Union
Today, READ MORE β†’
Fei toto kurejea kesho dhidi ya Geita Gold
Fei toto kurejea kesho dhidi ya Geita Gold
Today, READ MORE β†’
Yaya TourΓ© Aandika Historia UEFA Champions League, Awa mwafrika wa kwanza kufika hatua hii
Yaya TourΓ© Aandika Historia UEFA Champions League, Awa mwafrika wa kwanza kufika hatua hii
Today, READ MORE β†’
Yanga SC Wajipanga Vizuri kwa Mechi Dhidi ya Pamba Jiji
Yanga SC Wajipanga Vizuri kwa Mechi Dhidi ya Pamba Jiji
Today, READ MORE β†’
Liverpool Wakubaliana na PSG Kumsajili Bradley Barcola
Liverpool Wakubaliana na PSG Kumsajili Bradley Barcola
Today, READ MORE β†’
Timu zaidi zafuzu Champions League, droo ya msimu mpya kuchezeshwa leo.
Timu zaidi zafuzu Champions League, droo ya msimu mpya kuchezeshwa leo.
Today, READ MORE β†’
Mbappe aivunja rekodi ya Ronaldo ya mabao 86 misimu miwili Real Madrid
Mbappe aivunja rekodi ya Ronaldo ya mabao 86 misimu miwili Real Madrid
Yesterday, READ MORE β†’