Barcelona yamnasa Gabriel Jesus Kutoka Arsenal

Abdulrahman Said By Abdulrahman Said β€’ 30th August 2026


Barcelona yamnasa Gabriel Jesus Kutoka Arsenal

Barcelona imefikia makubaliano ya kushtukiza na Arsenal kwa ajili ya kumsajili mshambuliaji wa Brazil, Gabriel Jesus.

Jesus, mwenye umri wa miaka 29, anatarajiwa kusafiri kwenda Hispania mapema wiki hii kwa ajili ya vipimo vya afya, huku Arsenal ikiwa tayari imemruhusu kusafiri ili kukamilisha taratibu za uhamisho huo.

Barcelona inatarajiwa kulipa kiasi cha €10 milioni pamoja na nyongeza ili kumpata mshambuliaji huyo, ada ambayo ni ndogo ikilinganishwa na thamani yake ya soko inayokadiriwa kuwa kati ya €16 milioni na €17 milioni.

Usajili huo unakuja baada ya siku kadhaa za sintofahamu kuhusu mustakabali wa Jesus huko Arsenal, ambapo mshambuliaji huyo alikuwa nje ya mazoezi ya kikosi cha kwanza na alitarajiwa kuondoka klabuni hapo kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili.

Kwa mujibu wa Mundo Deportivo, usajili huo ulisukumwa na Mkurugenzi wa Michezo wa Barcelona, Deco, huku klabu hiyo ikitarajia kukamilisha dili hilo ndani ya saa 24 zijazo.


  

More Stories

United na Chelsea zavuruga raundi ya pili EPL
United na Chelsea zavuruga raundi ya pili EPL
Today, READ MORE β†’
Raja Casablanca yaingia katika mgogoro mkubwa, Nabi aondoka Casablanca
Raja Casablanca yaingia katika mgogoro mkubwa, Nabi aondoka Casablanca
Today, READ MORE β†’
Van Dijk amtaka Gakpo abaki Liverpool licha ya nia ya Manchester City
Van Dijk amtaka Gakpo abaki Liverpool licha ya nia ya Manchester City
Today, READ MORE β†’
Barcelona yamnasa Gabriel Jesus Kutoka Arsenal
Barcelona yamnasa Gabriel Jesus Kutoka Arsenal
Today, READ MORE β†’
Manqoba apania kuendeleza ubabe Yanga ikitua Arusha kuikabili Fountain Gate
Manqoba apania kuendeleza ubabe Yanga ikitua Arusha kuikabili Fountain Gate
Today, READ MORE β†’
Simba vs Geita Gold: Barker afunguka maandalizi
Simba vs Geita Gold: Barker afunguka maandalizi
Today, READ MORE β†’
Simba SC yaachana rasmi na Alassane KantΓ© baada ya msimu mmoja
Simba SC yaachana rasmi na Alassane KantΓ© baada ya msimu mmoja
Today, READ MORE β†’
Highlights : Singida BS 4-2 Polisi Tanzania
Highlights : Singida BS 4-2 Polisi Tanzania
Yesterday, READ MORE β†’
Ahmed Ally asema Simba ya sasa ni bora zaidi katika misimu mitatu iliyopita
Ahmed Ally asema Simba ya sasa ni bora zaidi katika misimu mitatu iliyopita
Yesterday, READ MORE β†’
NBC Premier League leo: michezo mitatu ya kibabe.
NBC Premier League leo: michezo mitatu ya kibabe.
Yesterday, READ MORE β†’