Nahodha wa Liverpool, Virgil van Dijk, amesema angependa mshambuliaji wa Timu ya Taifa hiyo na taifa la Uholanzi, Cody Gakpo, abaki Anfield licha ya taarifa za Manchester City kuonyesha nia ya kumsajili kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili.
Akizungumza baada ya Liverpool kutoka sare ya 2-2 dhidi ya Nottingham Forest, Van Dijk amesisitiza umuhimu wa klabu hiyo kuendelea kuwa na wachezaji wenye ubora, akimtaja Gakpo kama mchezaji muhimu kwa timu hiyo. “Ni mchezaji mwenye ubora. Nadhani tunapaswa kubaki na wachezaji wenye ubora,” alisema Van Dijk.
Taarifa zinaeleza kuwa Manchester City wako tayari kutoa hadi Pauni milioni 85 kwa ajili ya Gakpo, huku Liverpool wakitajwa kutokuwa tayari kumuuza bila kwanza kupata mbadala anayefaa. Liverpool pia wanaendelea na mipango ya kuimarisha safu yao ya ushambuliaji, ikiwa ni pamoja na mazungumzo yanayomhusu Bradley Barcola wa Paris Saint-Germain.



