Van Dijk amtaka Gakpo abaki Liverpool licha ya nia ya Manchester City

Abdulrahman Said By Abdulrahman Said β€’ 30th August 2026


Van Dijk amtaka Gakpo abaki Liverpool licha ya nia ya Manchester City

Nahodha wa Liverpool, Virgil van Dijk, amesema angependa mshambuliaji wa Timu ya Taifa hiyo na taifa la Uholanzi, Cody Gakpo, abaki Anfield licha ya taarifa za Manchester City kuonyesha nia ya kumsajili kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili.

Akizungumza baada ya Liverpool kutoka sare ya 2-2 dhidi ya Nottingham Forest, Van Dijk amesisitiza umuhimu wa klabu hiyo kuendelea kuwa na wachezaji wenye ubora, akimtaja Gakpo kama mchezaji muhimu kwa timu hiyo. “Ni mchezaji mwenye ubora. Nadhani tunapaswa kubaki na wachezaji wenye ubora,” alisema Van Dijk.

Taarifa zinaeleza kuwa Manchester City wako tayari kutoa hadi Pauni milioni 85 kwa ajili ya Gakpo, huku Liverpool wakitajwa kutokuwa tayari kumuuza bila kwanza kupata mbadala anayefaa. Liverpool pia wanaendelea na mipango ya kuimarisha safu yao ya ushambuliaji, ikiwa ni pamoja na mazungumzo yanayomhusu Bradley Barcola wa Paris Saint-Germain.


  

More Stories

United na Chelsea zavuruga raundi ya pili EPL
United na Chelsea zavuruga raundi ya pili EPL
Today, READ MORE β†’
Raja Casablanca yaingia katika mgogoro mkubwa, Nabi aondoka Casablanca
Raja Casablanca yaingia katika mgogoro mkubwa, Nabi aondoka Casablanca
Today, READ MORE β†’
Van Dijk amtaka Gakpo abaki Liverpool licha ya nia ya Manchester City
Van Dijk amtaka Gakpo abaki Liverpool licha ya nia ya Manchester City
Today, READ MORE β†’
Barcelona yamnasa Gabriel Jesus Kutoka Arsenal
Barcelona yamnasa Gabriel Jesus Kutoka Arsenal
Today, READ MORE β†’
Manqoba apania kuendeleza ubabe Yanga ikitua Arusha kuikabili Fountain Gate
Manqoba apania kuendeleza ubabe Yanga ikitua Arusha kuikabili Fountain Gate
Today, READ MORE β†’
Simba vs Geita Gold: Barker afunguka maandalizi
Simba vs Geita Gold: Barker afunguka maandalizi
Today, READ MORE β†’
Simba SC yaachana rasmi na Alassane KantΓ© baada ya msimu mmoja
Simba SC yaachana rasmi na Alassane KantΓ© baada ya msimu mmoja
Today, READ MORE β†’
Highlights : Singida BS 4-2 Polisi Tanzania
Highlights : Singida BS 4-2 Polisi Tanzania
Yesterday, READ MORE β†’
Ahmed Ally asema Simba ya sasa ni bora zaidi katika misimu mitatu iliyopita
Ahmed Ally asema Simba ya sasa ni bora zaidi katika misimu mitatu iliyopita
Yesterday, READ MORE β†’
NBC Premier League leo: michezo mitatu ya kibabe.
NBC Premier League leo: michezo mitatu ya kibabe.
Yesterday, READ MORE β†’