Ibrahim Doumbia aguswa na mapenzi ya mashabiki wa Simba, hadi machozi yamtoka.

Xtra 90 Media By Xtra 90 Media β€’ 1st September 2026


Ibrahim Doumbia aguswa na mapenzi ya mashabiki wa Simba, hadi machozi yamtoka.

Mshambuliaji wa Simba SC, Ibrahim Doumbia, ameguswa kwa kiasi kikubwa na upendo na sapoti aliyopewa na mashabiki wa klabu hiyo baada ya mchezo dhidi ya Geita Gold.

Doumbia amesema aliposhuka kwenye basi baada ya mchezo huo, aliona bango lililoandikwa “TUKO PAMOJA DOUMBIA, TUNAKUPENDA”, jambo ambalo lilimgusa sana moyoni na kumfanya machozi yamtoke.

Mshambuliaji huyo ameeleza kuwa ujumbe huo kutoka kwa mashabiki umempa nguvu na kumfanya ajione kuwa yupo sehemu ambayo anaaminiwa na kuthaminiwa na familia ya Simba.

Amesema anawashukuru kwa dhati mashabiki wa Simba pamoja na familia nzima ya klabu kwa sapoti, upendo na imani wanayoendelea kumpa, akiahidi kutorudisha nyuma jitihada zake.

Doumbia ameweka wazi kuwa ataendelea kupambana, kufanya kazi kwa bidii na kutoa kila alichonacho kila anapovaa jezi ya Simba, akiamini kuwa juhudi hizo zitasaidia kufikia malengo ya klabu.

Upendo ulioonyeshwa na mashabiki baada ya mchezo huo unaonekana kuwa ishara ya uhusiano mkubwa uliopo kati yao na mchezaji huyo, huku Doumbia akiahidi kuwalipa kwa matokeo na kujituma zaidi uwanjani.


  

More Stories

Pitso Mosimane atangazwa rasmi kuwa Kocha Mkuu wa Afrika Kusini
Pitso Mosimane atangazwa rasmi kuwa Kocha Mkuu wa Afrika Kusini
Today, READ MORE β†’
Ibrahim Doumbia aguswa na mapenzi ya mashabiki wa Simba, hadi machozi yamtoka.
Ibrahim Doumbia aguswa na mapenzi ya mashabiki wa Simba, hadi machozi yamtoka.
Today, READ MORE β†’
Keffe D apatikana na hatia ya mauaji ya Tupac Shakur baada ya miaka 30
Keffe D apatikana na hatia ya mauaji ya Tupac Shakur baada ya miaka 30
Today, READ MORE β†’
Agosti Yawaweka Kichwa kwa Kichwa Gueye na Nzengeli kwa Tuzo ya Mchezaji Bora
Agosti Yawaweka Kichwa kwa Kichwa Gueye na Nzengeli kwa Tuzo ya Mchezaji Bora
Today, READ MORE β†’
Mabula aibukia JS Kabylie
Mabula aibukia JS Kabylie
Today, READ MORE β†’
Yanga kuanza kampeni za kimataifa na jezi mpya
Yanga kuanza kampeni za kimataifa na jezi mpya
Today, READ MORE β†’
Waamuzi wanne kutoka Tanzania wateuliwa na CAF kuchezesha mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika
Waamuzi wanne kutoka Tanzania wateuliwa na CAF kuchezesha mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika
Today, READ MORE β†’
Waamuzi wa Tanzania kuchezesha JS Saoura dhidi ya Horoya
Waamuzi wa Tanzania kuchezesha JS Saoura dhidi ya Horoya
Today, READ MORE β†’
Uwanja ndio sababu hatufungi magoli mengi : Steve Berker Kocha wa Simba
Uwanja ndio sababu hatufungi magoli mengi : Steve Berker Kocha wa Simba
Today, READ MORE β†’
Mashabiki wa Simba wamgusa Doumbia kwa ujumbe wa upendo
Mashabiki wa Simba wamgusa Doumbia kwa ujumbe wa upendo
Today, READ MORE β†’