Chelsea yasalitiwa kwa lamine siku ya mwisho ya usajili

Abdulrahman Said By Abdulrahman Said β€’ 2nd September 2026


Chelsea yasalitiwa kwa lamine siku ya mwisho ya usajili

Chelsea wamekumbwa na pigo kubwa siku ya mwisho ya dirisha la usajili baada ya Monaco kuvunja dili la kumsajili kiungo Lamine Camara, licha ya makubaliano ya awali kati ya klabu hizo kuwa yamefikia hatua za mwisho.

Camara alikuwa tayari kufanyiwa vipimo vya afya na kusaini mkataba wa miaka sita na Chelsea, huku nyaraka za uhamisho wa thamani ya pauni milioni 47 zikidaiwa kuwa zimesainiwa. Hata hivyo, Monaco iliwaandikia Chelsea dakika za mwisho kuwa imeamua kusitisha uhamisho huo.

Uamuzi wa Monaco ulihusishwa na mabadiliko katika mpango wa mshambuliaji Folarin Balogun kuhamia Everton. Monaco ilifufua mazungumzo ya uhamisho huo na kuamua kumbakiza Camara, lakini dili la Balogun nalo lilishindikana baadaye baada ya mchezaji huyo kukataa kuhamia Everton.

Kuvunjika kwa dili hilo kumeiacha Chelsea bila muda wa kutosha kupata mbadala wa Camara, ambaye alikuwa akitarajiwa kusaidia kuziba pengo la Enzo Fernandez. Chelsea walikuwa wamekubali uhamisho wa Fernandez kwenda Manchester City kwa pauni milioni 125 na, licha ya kuwa na nafasi ya kuzuia mpango huo, wakaendelea na makubaliano yaliyofikiwa.


  

More Stories

Simba yatangaza ujio wa Simba marathon kwenye maadhimisho ya miaka 90
Simba yatangaza ujio wa Simba marathon kwenye maadhimisho ya miaka 90
Today, READ MORE β†’
Uganda U23 yajitoa kwenye mbio za kufuzu AFCON U23 2027
Uganda U23 yajitoa kwenye mbio za kufuzu AFCON U23 2027
Today, READ MORE β†’
Chelsea yasalitiwa kwa lamine siku ya mwisho ya usajili
Chelsea yasalitiwa kwa lamine siku ya mwisho ya usajili
Today, READ MORE β†’
CAF: Timu mwenyeji ndiye mwenye jukumu la urushaji wa matangazo ya mechi hatua za awali
CAF: Timu mwenyeji ndiye mwenye jukumu la urushaji wa matangazo ya mechi hatua za awali
Today, READ MORE β†’
Yanga na Simba zaweka hadharani viwanja vya nyumbani ligi ya mabingwa
Yanga na Simba zaweka hadharani viwanja vya nyumbani ligi ya mabingwa
Today, READ MORE β†’
Yanga SC wafika Johannesburg, waelekea Botswana kwa ajili ya mchezo wa CAF
Yanga SC wafika Johannesburg, waelekea Botswana kwa ajili ya mchezo wa CAF
Today, READ MORE β†’
Steve Barker atoa wasiwasi kuhusu hali ya Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo
Steve Barker atoa wasiwasi kuhusu hali ya Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo
Today, READ MORE β†’
CAF Champions League na Confederation Cup Zaanza Wikiendi Hii.
CAF Champions League na Confederation Cup Zaanza Wikiendi Hii.
Today, READ MORE β†’
Uwanja wa Uhuru waandaliwa tayari kuwa machinjio ya Simba kwenye CAF Champions League.
Uwanja wa Uhuru waandaliwa tayari kuwa machinjio ya Simba kwenye CAF Champions League.
Today, READ MORE β†’
Singida Black Stars Yaibuka na Ushindi, Yapanda Nafasi ya Nne NBC Premier League.
Singida Black Stars Yaibuka na Ushindi, Yapanda Nafasi ya Nne NBC Premier League.
Today, READ MORE β†’