Chelsea wamekumbwa na pigo kubwa siku ya mwisho ya dirisha la usajili baada ya Monaco kuvunja dili la kumsajili kiungo Lamine Camara, licha ya makubaliano ya awali kati ya klabu hizo kuwa yamefikia hatua za mwisho.
Camara alikuwa tayari kufanyiwa vipimo vya afya na kusaini mkataba wa miaka sita na Chelsea, huku nyaraka za uhamisho wa thamani ya pauni milioni 47 zikidaiwa kuwa zimesainiwa. Hata hivyo, Monaco iliwaandikia Chelsea dakika za mwisho kuwa imeamua kusitisha uhamisho huo.
Uamuzi wa Monaco ulihusishwa na mabadiliko katika mpango wa mshambuliaji Folarin Balogun kuhamia Everton. Monaco ilifufua mazungumzo ya uhamisho huo na kuamua kumbakiza Camara, lakini dili la Balogun nalo lilishindikana baadaye baada ya mchezaji huyo kukataa kuhamia Everton.
Kuvunjika kwa dili hilo kumeiacha Chelsea bila muda wa kutosha kupata mbadala wa Camara, ambaye alikuwa akitarajiwa kusaidia kuziba pengo la Enzo Fernandez. Chelsea walikuwa wamekubali uhamisho wa Fernandez kwenda Manchester City kwa pauni milioni 125 na, licha ya kuwa na nafasi ya kuzuia mpango huo, wakaendelea na makubaliano yaliyofikiwa.



