Shirikisho la Soka Afrika (CAF) limefanya ukaguzi wa miundombinu mbalimbali jijini Arusha ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Tanzania kuelekea fainali za AFCON 2027, ambazo Tanzania itaziandaa kwa pamoja na Kenya na Uganda.
Katika ukaguzi huo, CAF imepitia Uwanja wa Arusha, viwanja vya mazoezi pamoja na vituo muhimu vya huduma za afya na matibabu vinavyotarajiwa kuwa sehemu ya maandalizi ya mashindano hayo makubwa ya soka barani Afrika.
Ukaguzi huo unaendelea kuonyesha hatua zinazochukuliwa na Tanzania kuhakikisha miundombinu na huduma muhimu zinakidhi viwango vinavyohitajika na CAF kabla ya michuano hiyo kufanyika mwaka 2027.
Tanzania, kupitia ushirikiano wa pamoja na Kenya na Uganda, inaendelea na maandalizi ya kihistoria ya AFCON 2027, huku Arusha ikiwa miongoni mwa maeneo muhimu yanayotarajiwa kuwa sehemu ya maandalizi na utekelezaji wa mashindano hayo.
.jpg)
.jpg)



