Local, Normal News, CAF CL, Simba Sc, Mighty

Barker ataja mkakati wa ushindi Malawi

Joel JJ By Joel JJ
β€’
1h ago
Barker ataja mkakati wa ushindi Malawi

Kocha Mkuu wa Simba, Steve Barker, amesema kikosi chake kipo Malawi kikiwa na lengo la kuonyesha soka safi na kupata ushindi dhidi ya Mighty Wanderers katika mchezo wa hatua ya awali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Akizungumza na waandishi wa habari kuelekea mchezo huo utakaopigwa kesho Jumapili katika Uwanja wa Bingu, Barker amesema wanafahamu ubora wa wapinzani wao, akibainisha kuwa Mighty Wanderers ina wachezaji wenye uzoefu, wakiwemo wanaowakilisha timu zao za Taifa.

Hata hivyo, kocha huyo amesisitiza kuwa Simba ipo tayari kwa changamoto hiyo na inalenga kupata matokeo chanya yatakayoiweka katika nafasi nzuri ya kufuzu kwenda hatua inayofuata.

“Kila timu iliyoko kwenye michuano hii inataka kuvuka na kusonga mbele kama ilivyo kwetu Simba.”

“Mighty Wanderers ni timu nzuri inayoundwa na wachezaji wengi wenye uzoefu na wako katika timu zao za Taifa.”

“Lakini sisi tuko hapa kwa ajili ya kuonyesha soka safi na kupata matokeo chanya,” alisema Barker.

Simba yakamilisha maandalizi

Kikosi cha Simba kiliwasili Malawi jana na jioni kufanya mazoezi yake ya kwanza nchini humo ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea mchezo huo.

Leo, Wekundu wa Msimbazi wanatarajiwa kufanya mazoezi yao ya mwisho katika Uwanja wa Bingu.

Simba inalenga kuondoka Malawi ikiwa na matokeo mazuri ili kujipa nafasi kubwa ya kusonga mbele katika mashindano hayo ya juu ya klabu barani Afrika.

More Stories

Pacome atuma salamu Yanga kuelekea mchezo wa Gaborone united
Pacome atuma salamu Yanga kuelekea mchezo wa Gaborone united
1h ago
READ MORE β†’
Yanga yazindua tawi jipya Botswana, yaahidi ubingwa wa afrika
Yanga yazindua tawi jipya Botswana, yaahidi ubingwa wa afrika
2h ago
READ MORE β†’
Mnyama katika mtego wa Mighty Wonderers Jumapili
Mnyama katika mtego wa Mighty Wonderers Jumapili
3h ago
READ MORE β†’
Jkt tanzania na Pamba jiji kwenye vita ya alama leo
Jkt tanzania na Pamba jiji kwenye vita ya alama leo
5h ago
READ MORE β†’
Yanga mtegoni Botswana, kuikabili Gaborone United leo
Yanga mtegoni Botswana, kuikabili Gaborone United leo
7h ago
READ MORE β†’
Real Madrid na PSG zakutana na vipigo katika ligi zao.
Real Madrid na PSG zakutana na vipigo katika ligi zao.
15h ago
READ MORE β†’
Chama: Ilikuwa ngumu kucheza dhidi ya simba nikiwa na jezi ya timu nyingine
Chama: Ilikuwa ngumu kucheza dhidi ya simba nikiwa na jezi ya timu nyingine
17h ago
READ MORE β†’
Clatous Chama : Nilijutia kuondoka simba
Clatous Chama : Nilijutia kuondoka simba
17h ago
READ MORE β†’
Massanza akumbana na faini kamati ya saa 72
Massanza akumbana na faini kamati ya saa 72
1d ago
READ MORE β†’