Local, Normal News, Simba, Gueye, CAFCL, Mighty wanderers, Tanzania, Malawi

Simba kuikabili Mighty wanderers bila Libasse Gueye

Abdulrahman Said By Abdulrahman Said
β€’
3h ago
Simba kuikabili Mighty wanderers bila Libasse Gueye

Simba SC itakosa huduma ya mshambuliaji Libasse Guèye katika mchezo wa kwanza wa mzunguko wa awali wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Mighty Wanderers ya Malawi, utakaochezwa katika Uwanja wa Bingu National Stadium jijini Lilongwe.

Guèye hatakuwa sehemu ya kikosi cha Simba kutokana na kutumikia adhabu ya kadi nyekundu aliyoipata msimu uliopita katika mchezo wa hatua ya makundi dhidi ya Petro Atlético ya Angola. Kutokuwepo kwake kunaongeza changamoto kwa Simba katika maandalizi ya mchezo huo wa kimataifa.

Kwa upande wa Mighty Wanderers, Simba inakutana na klabu yenye historia kubwa katika soka la Malawi. Klabu hiyo iliyoanzishwa mwaka 1962 jijini Blantyre, ni miongoni mwa timu kongwe nchini humo na imeshinda ubingwa wa Super League ya Malawi mara saba.

Wanderers pia inaingia katika mchezo huo ikiwa na mabadiliko kwenye benchi la ufundi baada ya kumsimamisha kazi kocha wake mkuu, Bob Mpinganjira, siku chache kabla ya mchezo huo. Hatua hiyo imeifanya klabu hiyo kumteua kocha wa muda kuiongoza timu katika kibarua hicho dhidi ya Simba.

More Stories

Sele Gomez avuruga sherehe Gaborone United dakika za Jioni
Sele Gomez avuruga sherehe Gaborone United dakika za Jioni
15h ago
READ MORE β†’
Highlights : Gaborone United 1-1 Yanga
Highlights : Gaborone United 1-1 Yanga
16h ago
READ MORE β†’
Pacome atuma salamu Yanga kuelekea mchezo wa Gaborone united
Pacome atuma salamu Yanga kuelekea mchezo wa Gaborone united
23h ago
READ MORE β†’
Barker ataja mkakati wa ushindi Malawi
Barker ataja mkakati wa ushindi Malawi
23h ago
READ MORE β†’
Yanga yazindua tawi jipya Botswana, yaahidi ubingwa wa afrika
Yanga yazindua tawi jipya Botswana, yaahidi ubingwa wa afrika
1d ago
READ MORE β†’
Mnyama katika mtego wa Mighty Wonderers Jumapili
Mnyama katika mtego wa Mighty Wonderers Jumapili
1d ago
READ MORE β†’
Jkt tanzania na Pamba jiji kwenye vita ya alama leo
Jkt tanzania na Pamba jiji kwenye vita ya alama leo
1d ago
READ MORE β†’
Yanga mtegoni Botswana, kuikabili Gaborone United leo
Yanga mtegoni Botswana, kuikabili Gaborone United leo
1d ago
READ MORE β†’
Real Madrid na PSG zakutana na vipigo katika ligi zao.
Real Madrid na PSG zakutana na vipigo katika ligi zao.
1d ago
READ MORE β†’