International, Normal News, Tevez, Messi, Ronaldo, Argentina, Manchester united,

Tevez kuvunja mwiko, Messi na Ronaldo kucheza timu moja

Abdulrahman Said By Abdulrahman Said
1h ago
Tevez kuvunja mwiko, Messi na Ronaldo kucheza timu moja

Mchezaji wa zamani wa Manchester United na Juventus, Carlos Tévez, anapanga kufanya mchezo wake wa kuaga soka katika Uwanja wa La Bombonera, Argentina, mwezi Desemba 2026, miaka minne baada ya kutangaza kustaafu rasmi.

Katika mchezo huo, Tévez anatarajia kuwaalika baadhi ya mastaa aliowahi kucheza nao, huku Lionel Messi na Cristiano Ronaldo wakiwa miongoni mwa majina makubwa anayataka yashiriki katika tukio hilo. Tévez anataka kuwaona nyota hao wakicheza upande mmoja katika mchezo huo maalum.

Tévez amesema kuwa kuwaunganisha Messi na Ronaldo katika timu moja ni ndoto yake ya muda mrefu, akiamini tukio hilo litakuwa la kipekee kwa mashabiki wa soka duniani. Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa, nyota hao wawili tayari wamekubali kushiriki katika mchezo huo.

Tévez alicheza pamoja na Ronaldo akiwa Manchester United na Messi katika Timu ya Taifa ya Argentina. Pia aliitumikia Boca Juniors katika vipindi mbalimbali, akicheza jumla ya mechi 279 na kufunga mabao 94, huku La Bombonera ikiwa moja ya viwanja vyenye umuhimu mkubwa katika historia yake ya soka.

More Stories

Ziyech aagana na afrika, aanza safari mpya Brazil na Botafogo
Ziyech aagana na afrika, aanza safari mpya Brazil na Botafogo
1h ago
READ MORE →
UEFA Champion League kurejea kesho kwa Kishindo.
UEFA Champion League kurejea kesho kwa Kishindo.
3h ago
READ MORE →
Azam na Namungo kukipiga leo, Rekodi yawaumiza wageni
Azam na Namungo kukipiga leo, Rekodi yawaumiza wageni
3h ago
READ MORE →
Singida Black Stars wafika Uwanja wa Kimataifa wa Juba kurejea Dar es Salaam
Singida Black Stars wafika Uwanja wa Kimataifa wa Juba kurejea Dar es Salaam
5h ago
READ MORE →
Depu Azidi Kuwaka, akiipa Petro de Luanda Ushindi Ugenini.
Depu Azidi Kuwaka, akiipa Petro de Luanda Ushindi Ugenini.
5h ago
READ MORE →
Kamwe atangaza sele day kuingamiza Gaborone, mashabiki yanga watakiwa kuiga style yake
Kamwe atangaza sele day kuingamiza Gaborone, mashabiki yanga watakiwa kuiga style yake
7h ago
READ MORE →
Yanga inazidi kuimarika na tunataka ubingwa wa afrika : Manqoba
Yanga inazidi kuimarika na tunataka ubingwa wa afrika : Manqoba
7h ago
READ MORE →
Singida BS yaweka rekodi Afrika, yagawa dozi nene Sudan Kusini
Singida BS yaweka rekodi Afrika, yagawa dozi nene Sudan Kusini
8h ago
READ MORE →
EPL Updates: Everton na Arsenal Zang’ara Katika Michezo ya Leo.
EPL Updates: Everton na Arsenal Zang’ara Katika Michezo ya Leo.
18h ago
READ MORE →